Monday 30 April 2012

Na Gazeti la mwananchi: Mawaziri wagoma


MKULO ASEMA HAWAJIBIKI KAMATI KUU CCM, NUNDU ATOA MANENO MAKALI, MAIGE, "NIACHENI"

Rais Kikwete akifafanua jambo
Ramadhan Semtawa na Boniface Meena

SIKU chache baada ya Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kubariki uamuzi wa Rais Jakaya Kikwete wa kulisuka upya Baraza la Mawaziri kwa kuwaondoa waliotajwa katika Ripoti Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mawaziri wanaotakiwa kujiuzulu wamekataa kuchukua hatua hiyo huku mmoja wao, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema hawajibiki kwa chombo hicho cha chama.

Kwa wiki mbili sasa, kumekuwa na shinikizo la kutaka mawaziri wanane wajiuzulu nyadhifa zao kutokana na wizara zao kutajwa na CAG kwamba zimehusika na ufisadi huku wengine wakitajwa moja kwa moja kufanya uamuzi wenye maslahi binafsi.

Wakizungumza na waandishi wetu kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya mawaziri hao walisema wanaacha hatima yao mikononi mwa Rais ambaye ndiye mamlaka ya uteuzi na kutengua nafasi zao.

Mkulo
Mwandishi: Asalaam alaykum ndugu yangu Waziri Mkulo.
Mkulo: Walaykum Salaam.
Mwandishi: Habari ya mapumziko?
Mkulo: Aaah salama.

Mwandishi: Nimekupigia kutaka kujua msimamo wako kuhusu uamuzi wa CC.
Mkulo: Nakusikiliza endelea.

Mwandishi: CC imebariki Rais Kikwete afumue Baraza la Mawaziri ni kwa nini usijiuzulu kabla?
Mkulo: No comment, (sina la kusema).

Mwandishi: Lakini, CC ina nafasi kubwa katika utendaji wa Serikali, kwa nini huoni uzito wa agizo lake?
Mkulo: Mimi sijaona muhtasari wa vikao vya CC lakini, pia siwajibiki kwa CC.
Mwandishi: Kwa maana nyingine huwezi kujiuzulu?
Mkulo: No comment katika hilo.

Mkulo amekuwa akitajwa kutaka kuvunja Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) kwa madai ya kuficha kile kilichoitwa baadhi ya tuhuma za ufisadi katika uuzaji mali za umma ikiwemo Kiwanja Namba 10 kilichopo Barabara ya Nyerere, kwa Kampuni ya Mohamed Enterpises (MeTL).


No comments:

Post a Comment