Saturday 30 June 2012

HIKI NDICHO WANACHOKISEMA MADAKTARI BINGWA, SASA NI HATARI!!

TAMKO LA MADAKTARI MABINGWA WA MKOA WA DAR ES SALAAM
(MNH, MOI, OCEAN ROAD NA HOSPITALI ZA MANISPAA YA MKOA WA DAR ES SALAAM)


Kutokana na kikao kilichofanyika leo tarehe 29/06/2012, Madaktari mabingwa tumeamua yafutayo:

Tunalaani kwa kauli moja kitendo alichofanyiwa Daktari na Kiongozi wa Jumuiya yetu, Dkt. Steven Ulimboka, cha kutekwa, kuumizwa na kutupwa msitu wa Mabwepande. Kitendo hiki kimetuhuzunisha, kimetufadhaisha na kutufanya kuishia katika hofu ya hali ya juu.
Tunazitaka Mamlaka husika kutuhakikishia mustakabali wa usalama wetu sasa na siku za mbeleni katika nchi yetu.
Tunalaani juhudi zinazofanywa na wadhalimu wote katika fani ya Udaktari.
Tunalaani vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa Madaktari wenzetu sehemu mbalimbali kama Bugando, Dodoma na Mbeya pamoja na kwingineko.
Tunatamka wazi kuwa kitendo cha kuwafukuza, kuwanyima mishahara na haki nyingine za mwezi Juni, ni udhalilishaji na kinyume na amri ya mahakama.
Kutokana na vitendo vyote tajwa hapo juu, (yaani kutekwa na kuteswa kwa Dkt. Ulimboka, Unyanyasaji wa Madaktari wenzetu) na pia kutokana na ukweli kwamba hali ya Dkt. Ulimboka inazidi kudorora; vile vile kwa kuwa siku zote Serikali imekuwa ikikubali kuwa madai yetu ni ya msingi (lakini haiyatafutii ufumbuzi wowote), TUMEAMUA KUSIKISHA KUTOA HUDUMA KATIKA HOSPITALI ZOTE TUKAZOFNYIA KAZI, yaani Muhimbili, MOI, Ocean Road, Amana, Mwananyamala, n.k. hadi hapo madai yetu ya msingi yatakaposikilizwa na kutekelezwa.
Tunaomba Madaktari mabingwa wote hapa nchini watuunge mkono katika harakati hizi za kuboresha sekta nzima ya afya.

IMETOLEWA NA
DKT. C. MNG’ONG’O
MWENYEKITI WA MADAKTARI MABINGWA - KANDA YA DAR ES SALAAM

Source:wavuti.com

No comments:

Post a Comment