Monday 5 March 2012

MAITI AJALI YA KIBAHA WATAMBULIWA


MAITI za abiria waliopoteza maisha katika ajali ya mabasi mawili madogo wilayani Kibaha wametambuliwa na baadhi wameanza kuchukuliwa na ndugu zao kwa ajili ya mazishi.

Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani, Mkuu wa Upelelezi mkoani humo Evance Mwijage alisema kuwa majeruhi wanne kati ya 42 wamehamishiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili Dar es Salaam kwa matibabu zaidi.